Saturday, 24 February 2018

Exam Hacks and Cheatings

Some of Exams Hacks and Cheating that are not allowed in examination ground... please and please adhere it and be careful... Una Muda mchache sana wa Kuwa chuoni cheating zitakufanya ukose chuo na kujutia Maisha yako... trust yourself and stay confident... 

BEST WISHES COLLEAGUES.

Regards..! 
Deputy Minister Information and Communication 

Thursday, 22 February 2018

Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE)-mshindi wa tuzo ya chuo bora cha mwaka 2016 Tanzania, anawakaribisha waombaji (applicants) wenye sifa za kujiunga na chuo muhula mpya wa masomo mwezi wa Machi, 2018 na mwezi Septemba 2018 kwa programu za kutwa na jioni katika ngazi ya Astashahada (Certificate), Stashahada (Diploma), na Stashahada ya Uzamili (Postgraduate Diploma) katika kozi mbalimbali.
Programu hizi zinatolewa katika kampasi zote za chuo kama ifuatavyo:
A.     ASTASHAHADA (CERTIFICATE PROGRAMMES) NTA LEVEL 4 (MWAKA 1)
1.   Uhasibu (Accountancy)
2.   Usimamizi wa Biashara (Business Administration).
3.   Masoko (Marketing)
4.   Ununuzi na Ugavi (Procurement and Supplies Management)
5.   TEHAMA (Information, Communication and Technology (ICT) (Dsm na Dodoma Pekee)
6.   Mizani na Vipimo (Certificate in Metrology and Standardization) (Kwa Dsm Pekee) 
Sifa za Kujiunga
1.     Mwombaji awe amemaliza kidato cha NNE (IV) na kupata ufaulu wa angalau masomo 4 kwa kiwango cha kuanzia D (4D’s). 
Zingatia: Muombaji wa kozi ya Uhasibu anapaswa awe amefaulu (Form IV) Hesabu kuanzia  kiwango cha D. Na anaeomba Kozi ya Mizani na Vipimo awe amefaulu Hesabu au Fizikia kuanzia  kiwango cha D.
AU
2.     Awe amesoma na kuhitimu NABE II kwa ufaulu wa angalau alama 4
Ada ya Masomo
Ada ya masomo kwa Mwaka ni TZS 920,000/= isipokuwa kwa kozi ya TEHAMA (Information, Communication and Technology (ICT) ambayo ada yake ni Tshs. 1,220,000/= na Mizani na Vipimo (Certificate in Metrology and Standardization) ambayo ada yake ni Tshs. 853,000/=
B.     STASHAHADA (DIPLOMA PROGRAMMES) NTA LEVEL 5 – 6 (MIAKA 2)
1.   Stashahada ya Uhasibu (Diploma in Accountancy) 
2.    Stashahada ya Usimamizi wa Biashara (Diploma in Business Administration)
3.   Stashahada ya Ununuzi na Ugavi (Diploma in Procurement and Supplies)
4.   Stashahada ya Masoko (Diploma in Marketing)
5.   TEHAMA (Information, Communication and Technology (ICT) (Dsm na Dodoma Pekee)
6.   Mizani na Vipimo (Diploma in Metrology and Standardization) (Dsm Pekee)
Sifa za Kujiunga
1.     Mwombaji awe amemaliza kidato cha SITA (VI) na kupata ufaulu wa angalau Principal Pass Moja au Subsidiary Mbili katika masomo unganishwa (Combination subject). AU 
2.     Awe amesoma na kuhitimu Astashahada (Certificate) kutoka chuo kinachotambulika na NACTE katika fani zifuatazo:
· Usimamizi wa Biashara (Business Administration).
· Masoko (Marketing)
· Ununuzi na Ugavi (Procurement and Supplies Management)
· TEHAMA (Information, Communication and Technology (ICT)
Ada ya Masomo
Ada ya masomo kwa Mwaka ni TZS 1,100,000/= isipokuwa kwa kozi ya TEHAMA (Information, Communication and Technology (ICT) ambayo ada yake ni Tshs. 1,400,000/= na Mizani na Vipimo (Diploma in Metrology and Standardization) ambayo ada yake ni Tshs. 1,014,400/= 
C.     STASHAHADA YA UZAMILI (POSTGRADUATE DIPLOMA PROGRAMMES)
1.   Postgraduate Diploma in Project Management (PGDPM) – Mwanza pekee
2.   Postgraduate Diploma in Business Administration PGDBA) – Mwanza pekee
3.   Postgraduate Diploma in Human Resource Management (PGDHRM) – Mwanza pekee
4.   Postgraduate Diploma in Financial Management (PGDFM) – Mwanza pekee
5.   Postgraduate Diploma in Investment (PGDIn) – Mwanza pekee
 Ada ya Masomo:
Ada ya masomo kwa Mwaka ni TZS 1,800,000/=
Sifa za kujiunga na Postgraduate Diploma (PGD)
1.      Mwombaji awe amehitimu Shahada (Degree) au Stashahada ya juu (Advanced Diploma). AU
2.     Mwombaji awe na CPA au CPSP
D.      UTARATIBU WA KUTUMA MAOMBI/KUJIUNGA NA CHUO
Maombi yote ya kujiunga na chuo yanafanyika chuoni au kwa njia ya mtandao (Online Application) kupitia tovuti ya chuo www.cbe.ac.tz kwa gharama ya TZS 10,000 tu.
Chuo kimepata kuwa chuo bora cha mwaka kwa mwaka 2016. Njoo ujiunge na chuo bora kwa elimu bora.
ZINGATIA:
Ada italipwa kwa awamu nyingi kama itakavyo elekezwa. Hostel zipo kipaombele kitatolewa kwa watakaowahi kuja kuanza masoma.

E.    MAHALI TULIPO
2   Dodoma
Eneo la Makole pembezoni mwa barabara iendayo Dar es Salaam
S. L. P. 2077, Dodoma
Email: dir.dodoma@cbe.ac.tz Au Piga Simu: +255 26 2321200
Website:cbe.ac.tz/dodomacampus

Friday, 8 December 2017


Na; Dadil C.M
Ilikuwa wakati wa Mechi kati ya Timu ya Basketball Team Red na Team Black. wadau hawa walijitokeza Kushangilia baada ya Goli kupatikana katika Ligi ya Chuo ya Chuo ijulikanayo kama CAC League 2017.... 

COBESO Annual Competition League 2017

Classroom 2017


Na; Dadil C.M 
Wanachuo wakiwa katika moja ya Vipindi vyao Computer Lab ya Chuo Cha CBE Dodoma
Katika kujifunza zaidi Computer Knowledge katika masomo ya Biashara yanayotolewa Chuoni Hapo..

CBE Dodoma Leaders in Business Education.

Via;
COBESO Dodoma 2017/18

Wednesday, 22 November 2017

Diploma II CAC League 2017

Wanachuo wa Diploma II wakiwa kwenye maandalizi ya mwisho kuelekea Ufunguzi wa Ligi ya Chuo Ijulikanayo kama CAC League 2017..

Katika Mechi ya Ufunguzi iliyochezwa Siku ya tar 21 Nov 2017 wanafunzi  wa Diploma II Waliibuka na Ushindi Mnono wa Goli 4 dhidi ya Bachelor 1

CAC League 2017


Wanachuo wa Bachelor 1 wakiwa kwenye maandalizi ya Mechi ya Ufunguzi wa Ligi ya Chuo ijulikanayo kama COBESO Annual Competition League (CAC League) 2017.

Katika Mechi hiyo wanafunzi wa Bachelor 1 walipokea kipigo cha Goli 4-1 Kutoka kwa Diploma II

Monday, 20 November 2017

Mahafali 2017


Wanachuo wa Diploma Wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kutunukwa stashahada zao, tukio hilo lilitokea siku ya tarehe 18.11.2017 Siku ya Jumamosi katika mahafali ya 52 ya chuo cha Elimu ya Biashara campus ya Dodoma. 

Sherehe hiyo ya Mahafali ya 52 ya chuo cha Elimu ya Biashara ilihudhuliwa na wadau mbalimbali kutoka serikalini, pamoja wageni kutoka sehemu mbalimbali pamoja na wandishi wa Habari...

Imetolewa na;

Dadil C.M
Naibu waziri wa Habari na mawasiliano
COBESO 2017/18

Friday, 17 November 2017

COBESO Dodoma News

I am Highly esteemed to welcome you to the second issue of COBESO Dodoma Campus, this issue presents some events and current success of COBESO with the goal of informing others on the development of COBESO Dodoma.

As you take time to read and pass through this issue let us continue to support COBESO for the walfare of the students and excellence..


Regards!  

DADIL C.M
Deouty Minister of information and Communication.
COBESO 2017

Wednesday, 15 November 2017

GEPF and COBESO Dodoma


Baadhi ya Viongozi wa serikali ya wanafunzi katika Picha ya pamoja na viongozi kutoka GEPF na Staff kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara mara baada ya tukio la makabidhiano ya vifaa vya Usafi wa Mazingira.. 

Vifaa vilivyotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa GEPF Kupitia wizara ya Afya, Mazingira na Jinsia kwa Ajili ya Chuo cha Elimu ya Biashara Dodoma.

Imetolewa na;

Dadil C.M
Naibu waziri wa Habri na Mawasiliano

Makabidhiano ya Vifaa vya Usafi


Raisi wa Serikali ya Wanafunzi CBE Dodoma Mhe, Brian L. Kifanga akipeana mkono na Meneja wa GEPF Kanda ya Kati Mr. Josephat Mshana wakati wa Makabidhiano ya vifaa vya Usafi vilivyotolewa na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii GEPF kwa kushirikiana na Serikali ya wanafunzi COBESO Dodoma ikiwa ni sehemu ya Kuunga Mkono Sera ya Mhe, Raisi wa Serikali ya Wanafunzi CBE Juu ya Uhifadhi wa Mazingira pamoja na kuwa na Mazingira safi. Makabidhiano hayo yalifanyika siku ya Ijumaa Tarehe 10 Mwezi wa 11. 2017 Katika Chuo cha elimu ya Biashara Dodoma.

Makabidhiano hayo yalishirikisha Baadhi ya Staff Kutoka GEPF Pamoja na Staff Kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara Dodoma na Viongozi kutoka serikali ya wanafunzi chini ya wizara ya Afya, Mazingira na Jinsia.

Kama Serikali ya Wanafunzi Tunapongeza Jitihada zilizofanywa na Wizara Husika pamoja na GEPF Kwa ajili ya Vifaa hivyo ambavyo vitaongeza tija katika Chuo chetu.


Imetolewa na;

Dadil C.M
Naibu waziri wa Habari na Mawasiliano

Friday, 13 October 2017

ORODHA YA MAJINA YA WANAFUNZI WATAKAOFANYA MAHAFALI CHUO CHA ELIMU YA BIASHARA DODOMA

Tembelea tovuti ya chuo ili kuona Orodha ya majina ya watakaofanya mahafali mwezi November Mwaka huu..Kwa Wanafunzi wa NTA Level 4, 6, & 8.
https://www.cbe.ac.tz

Tuesday, 26 September 2017

Release of Bachelor and Postgraduate supplimentary results.

 Taarifa Rasmi.
Matokeo ya supplimentary yanatarajiwa kutolewa tarehe 28 september kwa mujibu wa almanac ya chuo chetu, hivyo basi ni siku mbili tu zimebaki kuanzia sasa ili matokeo hayo yatolewe.
Tuendelee kuomba Mungu ili matokeo yawe mazuri kwa kila mmoja wetu.
Kama kuna tatizo/ shida fika ofisi ya COBESO tukuhudumie.